<p>Katika miaka zaidi ya 20 ya kufundisha Kiswahili kwa wageni sija-kutana na andiko la hadithi nzuri kama hizi alizoandika mwandi-ihi Marc Eichen. Ufundi wake wa kutumia vitushi halisi na kuvis-ana kwa maumbo mbalimbali ya lugha ni wa kipekee! Hadithi tatu hizi ni mchango mkubwa katika ufundishaji wa Kiswahili na fasihi kwa wenyeji na ugenini. Zitawasaidia pakubwa walimu pamoja na wanafunzi kufahamu uhondo wa lugha za Kiswahili na Kiingereza kupitia vipengele mbalimbali vya lugha aliyotumia mwandishi. Ndugu Suleiman Khalfan na Abdulrahman Ndegwa vilevile wametoa tafsiri ya haki wakilenga kabisa alichodhamiria mwandishi wa hadithi zenyewe.</p><p><br></p><p>- Dr. David Kyeu</p><p>Coordinator and Continuing Lecturer</p><p>Center for African Studies</p><p>University of California Berkeley</p><p><br></p><p>Hadithi katika kitabu cha Upepo Mchanga Anga ni fupi lakini zenye maana. Hadithi hizi zimejikita katika mandhari ya visiwa vya Zanzibar Afrika Mashariki taswira hizi za wazi zinamwalika msomaji kuandamana na wahusika wanaopitia changamoto za kibinafsi ndani ya eneo linalobadilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya kijamii na kiuchumi utalii na hata mabadiliko ya tabianchi. Kitabu hiki kita-wavutia wanafunzi wa Kiswahili na Afrika Mashariki kwa ujumla na kwa upana zaidi wale wanaotaka kuelewa mivutano ya kitamaduni na mabadiliko yanayohusiana na utandawazi.</p><p><br></p><p>- Caitlyn Bolton PhD Chuo cha Boston</p>
Piracy-free
Assured Quality
Secure Transactions
Delivery Options
Please enter pincode to check delivery time.
*COD & Shipping Charges may apply on certain items.