<p>Kitabu Uumbaji wa Mtu; kinaanzia na YAHWEH Katika Milele kuchambua yapi na vipi vilipelekea kuumbwa kwa ulimwengu na hatimaye pawepo mahali wakati ambapo mtu angeweza umbwa na kuishi humo. Ndipo tunaonyeshwa Kuumbwa kwa Roho na Nafsi ya Mtu katika milele kabla kabisa ya Kufanywa kwa Mwili Mme na Mke kwa minajili ya mtu katika hali ya roho-nafsi ahifadhiwe humo.</p><p>Mpango wa Ukombozi unaonyeshwa kama matokeo ya kuhakikisha uhitaji wa Mungu YAHWEH kuwa na familia unakamilika. Na hili lilijulikana na kupangwa kabla ya uanguko wa mtu duniani. Hivyo tokea ufahamu huu tunachungua kwa kina Tafsiri na Asili ya Uasi na Dhambi na hususani Kudanganywa kwa Havaa (Eva) na Uafiki wa Adam. Kuhitimisha haya yote tunafanyia uhakiki Dhana ya Dhambi ya Asili. Pamoja na haya ni mengi mengine ya kushangaza na kustaajabisha kuhusu Uumbaji wa Mtu.</p><p>Katika haya tunajibu sababu ya uwepo wako hapa duniani na maalumu kabisa ni yapi ndiyo wajibu na majukumu yako kama mtu. Na bila kupoteza muda tunafanyia mapitio nadharia kadhaa za uumbaji kuthibitisha kweli ya maandiko matakatifu. Kitabu chafaa sana kwa Mafundisho ya kitaaluma.</p>
Piracy-free
Assured Quality
Secure Transactions
Delivery Options
Please enter pincode to check delivery time.
*COD & Shipping Charges may apply on certain items.